Wataalam
kutoka chuo kikuu cha Kilimo Sokoine kilichopo Mkoa wa Morogoro (SUA)
wamesambaza mbegu bora za Maharage zaina
ya aina tano katika Halmashauri ya
Wilaya ya Siha .
Mbegu hizo bora
za Maharage zimefanyiwa utafiti katika
kituo cha Lyamungo na Emmaus kwa Masista na kuonekana kuwa na mafanikio
makubwa.
waliopatiwa mbegu hizo ni pamoja na Watendaji wa Vijiji,Maafisa
Ugani,Baadhi ya watumishi katika Idara ya Kilimo na Ushirika pamoja na Baadhi
ya waheshimiwa Madiwani na kutakiwa na Wataalam hao kuwa mfano kwa Wakulima
Wengine.
No comments:
Post a Comment